• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
MISSENYI DISTRICT COUNCIL
MISSENYI DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Missenyi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara na Vitengo
      • Idara ya Utawala na Utumishi
      • Idara ya Kilimo Ushirika na Umwagiliaji
      • Idara ya Mifugo na Uvuvi
      • Idara ya Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Afya na Ustawi wa Jamii
      • Fedha na Biashara
      • Idara ya Elimu Msingi
      • Idara ya Elimu ya Secondari
      • Idara ya Ujenzi
      • Idara ya Maji
      • Idara ya Ardhi na Maliasili
      • Idara ya Mipango Takwimu na Uuatiliaji
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Sheria
      • Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani
      • Kitengo cha Manunuzi na Ugavi
      • Kitengo cha Uchaguzi
      • Kitengo cha Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya Watalii
    • Kilimo
    • Uvuvi
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Madiwani
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Huduma za Kiuchumi
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
      • Kamati ya Kudhibiti ukimwi
    • Ratiba
  • Miradi
    • Itakayo Tekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa wateja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha mbalimbali

UZINDUZI WA WIKI YA KAGERA WAZIRI MKUU ASIFIA MAANDALIZI-AWAPA KONGOLE WANAKAGERA

Posted on: August 14th, 2019
  • Taarifa kwa hisani ya RS-Kagera


Nimehudhuria makongamano ya uwekezaji katika mikoa sita lakini kwa mkoa wa Kagera kweli mmejipanga kuhamasisha uwekezaji maandalizi yenu si ya michezo mnaye mkuu wa mkoa mbunifu na mfatiliaji, nimepita kwenye mabanda nimejionea bidhaa mbalimbali zinazosindikwa hapa Kagera kweli Kagera kwa mkakati huu mtafanikiwa.

Maneno hayo yalisemwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Kagera Agosti 14, 2019 katika viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Bukoba alipokuwa mgeni rasmi na kuzindua rasmi Wiki ya Uwekezaji Kagera.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Kagera alisema kama mkakati wa Wiki ya Uwekezaji Kagera utatumika vizuri utaupandiusha uwezo wa kiuchumi wa mwananchi mmoja mmoja, uwezo wa mkoa pia na Taifa kwa ujumla.

“Kama tutachangamkia fursa ya uwekezaji Kagera tutaweza kuinua zaidi pato la sasa la mwananchi ambapo kwasasa ni shilingi 1,370,000/= kwa mwaka na pato la mkoa la sasa la shilingi bilioni 4.98 aidha, mkoa wa Kagera utachangia zaidi pato la taifa badala ya asilimia 3.9 unavyochangia sas.” Alifafanua Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwahutubia wananchi pamoja na wageni mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara kutoka nchi za Burundi na Rwanda alisema kuwa kuna sababu za kuwekeza katika mkoa wa Kagera kwa sasa na alizitaja sababu hizo kama ifuatavyo:

Kwanza Mkoa wa Kagera una amani na utulivu na usalama wa kutosha ambapo alisema kuwa mwekezaji yeyeyote anapenda sana kuwekeza sehemu na mahala penye utulivu. Pili ni fursa za masoko katika mkoa wa Kagera ambapo alisema kuwa mkoa unapakana na nchi nne za Burundi, Rwanda, Kenya na Uganda lakini pia upo karibu na nchi za Kongo (DRC) na Sudani ya Kusini na kwa ujumla nchi hizo kuna soko la watu zaidi ya milioni 190.

Sababu ya tatu mkoa wa Kagera una hali nzuri ya hewa, ukiwa na rutuba ya kutosha kuotesha na kustawisha mazao yote, ukipata mvua nyingi mara mbili kwa mwaka kuanzia kwa kiwango cha milimita 600 hadi 2000 kwa mwaka. Kutokana na hali hiyo mkoa wa Kagera unaongoza kwa uzalishaji wa kahawa yenye ubora na pendwa sana duniani ya robusta na arabika.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa aliwasistiza wafanyabiashara kuja kuwekeza Kagera kwani viwanda vya kuchakata kahawa bado ni vichache sana lakini pia aliwakumbusha wananchi kuanza kuwekeza katika viwanda vidogo na vya kati kusindika mazao mbalimbali na kutolea mfano wa mjasiliamali wa anayetengeneza sabuni kwa mafuta ya mawese kutoka Wilayani Biharamulo anayezalisha boksi 2000 kwa mwaka.

Waziri mkuu Mhe. Kassim Majaliwa aliwasisitiza wafanyabiashara kutoka nchi jirani kuja Kagera kuwekeza katika kilimo cha zao la Vanilla ambalo linalipa sana na maka jana 2018 kilo moja ilikuwa inauzwa kwa shilingi 150,000/=.

Aidha, alisema kuwa Mkoa wa Kagera ni mkoa wenye neema kwani kuna fursa za kuwekeza katika uvuvi, maeneo ya kufugia katika ranchi za taifa ambako kuna zaidi ya hekta 120,000 za kufugia , vile vile alitoa wito kwa Wanankagera pamoja na Watanzania kuchangamkia fursa ya utalii hasa kujenga Mahoteli na kuanzisha makampuni ya utalii ili kuchangamkia fursa ya mbuga za Hifadhi za Taifa za Brigi Chato, Ibanda, na Rumanyika.

Naye Mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti wakati akitoa neno kabla ya Waziri Mkuu kuwahutubia wananchi alisema kuwa Kagera inawakalisha ukanda wa Kasikazini Magharibi kwa fursa ulizonazo na kuwa kitovu cha biashara kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati. Pia alimweleza Waziri Mkuu kuwa mara baada ya kukutana na Mabalozi wa nchi tano mkoa umejipangia kwenda katika nchi hizo kuhakikisha fursa zilizowasilishwa na Mabalozi hao zinafanyiwa kazi ili kuufungua uchumi wa ukanda wa Kasikazini Magharibi.

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akikamilisha hotuba yake aliwataka Wakuu wa mikoa wengine kuiga katika mkoa wa Kagera namna ya kutangaza fursa za uwekezaji na kuwahamasisha wawekezaji kuja Kagera kuwekeza kwani panafikika kwa njia zote za anga, barabara, na majini.

Mara baada ya hotuba yake Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa alizindua rasmi Wiki ya Uwekezaji Kagera , pili alizindua Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera na alizindua rasmi Kongamano la kujadili na kudadavua fursa za uwekezaji Kagera ambalo litaanza rasmi Agosti 15, 2019 wakati wote huo maonesho ya bidhaa mbalimbali yakiendelea katika viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Bukoba.

Tarifa Kwa Umma

  • MATOKEO KIDATO CHA NNE 2020 January 16, 2021
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI ZA MUDA September 21, 2020
  • ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA KWANZA 2021 MISSENYI December 19, 2020
  • MATOKEO KIDATO CHA SITA 2019 July 09, 2019
  • Tazama zote

Habari mpya

  • HALMASHAURI YATOA MKOPO WA TSH. 92,150,000.00 KWA VIKUNDI 15 VYA VIJANA NA WANAWAKE

    October 23, 2020
  • TIMU YA MENEJIMENTI YA HALMASHAURI YAKAGUA MIRADI 17 YA MAENDELEO INAYOTEKELEZWA NDANI YA HALMASHAURI

    October 15, 2020
  • HALMASHAURI YATOA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVu

    September 05, 2020
  • KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI AZINDUA RASMI UJENZI WA MRADI WA MAJI WA KYAKA-BUNAZI

    June 01, 2020
  • Tazama zote

Video

Video nyinginezo

Kurasa za Haraka

  • Historia
  • Dira na Dhima
  • Sheria ndogo za Halmashauri

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Mkoa Kagera
  • Tovuti ya Ajira
  • Wakala wa Serikali Mtandao
  • Tovuti ya Serikali Kuu
  • Tovuti ya TAMISEMI

Watembeleaji walipo

world map hits counter

Waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    BUNAZI MISSENYI KAGERA TANZANIA

    Sanduku la Posta: P.O.BOX 38 KYAKA MISSENYI

    Namba ya Simu ya mezani: 0732983531

    Namba ya simu :

    Barua pepe: ded@missenyidc.go.tz

Anuani zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki @2017 Wilaya ya Missenyi. Haki zote zimehifadhiwa